Wednesday, April 23, 2014

Namna mwanafunzi navyoweza kujiongezea uelewa na kumbukumbu



 Tatizo la wanafunzi wengi siku hizi wamekuwa na mtindo unaoitwa ‘copy and paste’ yaani anachofundishwa ndicho wanachokishika na wakati mwingine kukiandika, jambo ambalo huchagia kuwafanya wanafunzi washindwe kuwa ufahamu wa kutosha juu ya mambo wanayoyasoma.
 Katika hali ya kawaida kazi kubwa ya mwalimu ni kumpa mwanafunzi moja kati ya mambo manne yanayokamilisha pembe nne za kuta ya ufahamu.

 Hii ina maana kwamba mwanafunzi anayepewa moja na mwalimu hawezi kuwa imara kama yeye mwenyewe hakujenga kuta zake tatu za kujielewesha.

Haifai kuwa mwanafunzi mwenye mfano wa kasuku, kuiga kilichofanywa na mwingine. Lazima katika kila unachofundishwa uhakikishe kuwa unapata muda wa kukichambua kwa kina na kuzidi kujielewesha zaidi ya pale alipoishia mwalimu.

Njia pekee ya kufikia kiwango cha juu cha uelewa ni pamoja na kupata muda wa kuchambua na kutafiti kile ulichofundishwa na kupata muda wa kuwashirikisha wengine kile unachokijua zaidi ya ulichofundishwa darasani.

Mwanafunzi ambaye atakuwa na tabia ya kuwaleza au kuwafundisha wenzake anachokijua zaidi kuhusu jambo fulani ndiyo atakuwa anajijengea uwezo wa kufahamu zaidi na kuimarisha kumbukumbu za kile alichofundishwa.

Kilio cha wanafunzi wengi siku hizi ni usahaulifu. 
Ukichunguza kwa makini utagundua kuwa, usahaulifu huo unatokana na tabia ya kukariri kama kasuku na kutokuwa na muda wa kushirikiana na wenzake katika mijadala ya kujielemisha.

Nashauri kila unachojifunza pata muda wa kukichambua kwa kina na pendelea zaidi kuwafundisha na wengine juu ya kile ulichopata katika kujielimisha kwako. Ukifanya hivyo utaongezeka kimaarifa kila siku na hutasahau ulichofundishwa. Wazungu husema:  "The miracle is this – the more we share, the more we have."

No comments:

Post a Comment