Thursday, January 22, 2015

Vishawishi vya kimapenzi kwa wanafunzi na jinsi ya kuvishinda



Kwenye moja ya mada ya zangu kuhusu vizuizi vya mafanikio ya kimasomo tumeona suala la mwanafunzi kujihusisha na mapenzi limechukua nafasi ya pili, hii ina maana kuwa wanafunzi wengi hupoteza mwelekeo wa kimasomo baada ya kujiingiza katika ulimwengu wa mapenzi.

Jambo baya kabisa kwa wanafunzi ambao ni wenyeji wa masuala ya kimapenzi hivi sasa hasa wanawake ni kutokukumbuka namna walivyotekwa kimapenzi na wengi kati yao wanadai kuwa haukuwa utashi wao na kwamba walilazimishwa, aidha na watu, mazingira au misisimko ya miili, jambo ambalo si la kweli kisaikolojia.

UBAYA NI KIOO; UNAOUONA KWA WENZAKO NI WAKO



Watu wengi huhangaika sana kujua kama wanaifurahisha jamii au wanaiudhi. Wengine wamefikia hatua ya kujiuliza, wamekosea nini watu wanaowazunguka  mpaka wakajikuta wamechukiwa?  Kisaikolojia fikra za namna hii, ni  sawa na kutafuta gari kwenye mwanga kwa njia ya kupapasa!
“Nashanga mama mdogo ananichukia bure,  tena hakuna kosa nililomfanyia lakini hanipendi tu” Je wewe nawe umekuwa miongoni mwa watu wanaodhani unachukiwa bure?
Achana na hulka hiyo, hebu tambua ubaya wako kwa kuangalia vidokezo vifuatavyo, ambavyo naamini ukivisoma kwa umakini utagundua ni wapi unakosea hadi kufikia hatua ya kuchukiwa katika jamii.

Jambo gani ni muhumu; kupenda au kupedwa?



UCHUNGUZI unaonesha kuwa, watu wengi waliopata kuulizwa swali lililopo kwenye kichwa cha makala haya walipendelea zaidi kupendwa.
Ni nadra sana mtu kujinung’unikia juu  ya udhaifu wa kutopenda, kuliko lawama za kuwalaumu wengine kuwa hawampendi.

Tuesday, January 20, 2015

MNAWAFELISHA WAWE MAHAUSIGELI NA MAHAUSIBOI WENU




ENZI za mkoloni ambazo Mkuu wa Kaya nilikuwepo; mpango mahususi ulikuwa  elimu bora ni kwa watu weupe.
Weusi hawapekuwa nafasi kwenye shule bora kwa kuwa mkakati uliwataka waendelee kuwa mbumbumbu ili wawe watumwa katika mashamba ya mkonge na katani.

AVUNJIKA TAYA, AOMBA MSAADA WA 60, 000/= ATIBIWE

Emmanuel Nelson akiwa wodini Hospitali ya  Taifa Muhimbili.
EMMANUEL NELSON mwenye umri wa miaka kati ya (30 au 35, ambaye ni  mzaliwa wa Mbamba Bay, Ruvuma, na ambaye wazazi wake wanaishi Dodoma, anaomba msaada wa kutibiwa taya ambalo limevunjika.

WAZIRI AWAOMBA RADHI WANAFUNZI KENYA

Waziri wa Usalama nchini Kenya, Joseph Nkaissery.
Waziri wa Usalama nchini Kenya Joseph Nkaissery amewaomba radhi wanafunzi wa shule ya msingi waliofyatuliwa gesi ya kutoa machozi wakati walipokuwa wakiandamana kupinga unyakuzi wa kipande cha ardhi ambacho kilikuwa uwanja wao wa kuchezea.

Wanafunzi waliofyatuliwa gesi ya kutoa machozi kwa kuandamana kupinga unyakuzi wa uwanja wao.
Bwana Nkaissery amempa siku moja mnyakuzi wa ardhi hiyo kuondoa sehemu ya ukuta iliobaki baada ya wanafunzi kuuangusha na kisha kuondoka katika eneo hilo.

Wanalilia mali za wageni kuliko vifo vya wananchi!




PICHA ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama, iliyochapishwa hivi karibuni kwenye vyombo vya habari ikimuonesha akilia mbele ya mali za mwekezaji zilizoharibiwa na wafugaji sikuipenda.