Monday, April 4, 2011

Sifa10 za mpenzi/rafiki wa kweli



1- Mpenzi/rafiki wa kweli ni yule ambaye hatangoja kujua nini unahitaji yaani hana sababu ya kusubiri kuombwa ndiyo asaidie au atoe.

2 - Ni yule atakayejua wakati gani huna furaha au una furaha na atakuwa na wewe kwa hali zote mbili .

3 - Ni yule atayekuwa tayari kukusikiliza kwa kile utakachosema, hatojali umeongea baya au zuri .

4 -Atakuwa na wewe wakati wa shida na raha. Hatakuacha mtu wa kuvizia vizia na kujisogeza wakati ukiwa na raha.

5 – Mpenzi/rafiki wa kweli atakuheshimu na hatopenda kuwa nyuma na kukuacha bila msaada .

6 – Mpenzi/rafiki wa kweli ni yule atakayekupenda kwa moyo wake wote na wala si kwa ajili ya shinikizo fulani (pesa au mali)

7 – Mpenzi/rafiki wa kweli ni yule atakayeonyesha kuthamini nafasi yako kama rafiki au mpenzi mbele ya wengine

8 - Kwenye ukweli mpenzi mzuri atasema bila kukuficha na atapenda kukuonyesha mifano ya namna ya kuwa mkweli .

9 -Mpenzi/rafiki wa kweli ni yule anayejiamini, asiyeyumba katika maamuzi hata kama atalazimika kufanya maamuzi magumu .

10 - Atakuwa tayari kuvumilia hatakuwa mwepesi wa hasira wala kutumia lugha chafu au ubabe. Ni hayo tu jipeme na umpime umpendaye!

No comments:

Post a Comment